Friday, 23 November 2012

KWENU KUNA STIMA?(SPOKENWORD POEM)



Kila Usiku wa jana upitao,
Unaniacha Mwenzenu na Mzigo kibao,
Mzigo wa hasira Moyoni Ninao,
Japo kila kuchao najilazimisha kusahau,
Wakifungua vinywa vyao wadau,
Hawafanyi lolote zaidi ya kunikumbusha,
Mimi ndo kitoweo chao,
Natumika kama mpira sababu,
Maishani sina dira,
Naamini aliyeniambukiza huu ujinga,
Ana uhusiano na mganga anayetaka kuniganga,
Utaniambiaje wakimwaga mboga nimwage ugali,
Wakati chakula chao ni maziwa na asali?,
One, two, one, two, wanaandaa vipaza,
Wakisubiri giza limeze mwangaza,
Ili vifo vyetu waje kuvitangaza,
Ajabu naogelea kwenye damu bila kujali
Alichinjwa nani,nikielezwa marehemu
Alinitanguliza nataka kubisha haiwezekani,
Mwanasiasa hivi we umetumwa na nani?,
Mbona uwe kama balozi wa Shetani?,
Vijana imewashinda kutumia bongo zao
Kwetu kuna giza kibao.,
Kwenu kuna stima?

No comments:

Post a Comment