NATONGOZA
PESA
//Mara ya kwanza mi nakuona,aki ya nani mi sikuamini//
//Nilikutamani ile kwa saana,hata kama haukuvalia
mini//
//Wish ungekisoma, kitabu changu cha moyoni//
///Mwenyewe ungeona, kilichoandikwa kwa zako mboni//
//Nikajiuliza mbona, nisikutongoze uingie kwangu mfukoni//
//Siku zikapita,nikapelekwa darasani//
//Ulikua tu unapita, hujali hata mi ni nani//
//Everyday it was ,my desire to be with you//
//Simply because, couldn’t make it
without you//
//Namix English na Kiswahili, usishangae kwa nini//
//Nakuonyesha umahiri,usione taabu kuwa na mimi//
//Nakuomba tu collabo, uje kwangu mfukoni nikuweke//
//Japo tufanye mambo, kuufukuza umaskini hadi kieleweke//
//Nitakuficha popote, ili mradi tu nisikupoteze//
//Ukianguka nikuokote, fasta kabla umaskini unichokoze//
//Nahitaji kuwa na wewe, ili nipewe heshima kitaa//
//Nakuomba pliz unielewe, bila we waschana washanikataa//
//Nipunguzie mavazi kuchakaa, na watu kunishangaa//
//Nitachoma hata mkaa,ndo niwe na wewe, mwaaaaaaa!!!!//
No comments:
Post a Comment